TAMATI YA MTUNZI
TAMATI YA MTUNZI.
Josephat S. Hema
Laiti
ningalijua,kutunga japo utenzi,
Sifa
ningemwagia,japo wengi wamuenzi,
Sana
ningemsifia,alivyokuwa kipenzi,
Daima
tamlilia,tamati yake mtunzi.
Pale
alipoishia,alionesha ujuzi,
Kalamu
akaachia,ilipomwishia pumzi,
Huku
tukimwangalia,ilo bora yake kazi,
Wote
tuliobakia,kumuiga hatuwezi.
Yale
maneno sawia,aliyoyaweka wazi,
Wino
katuandikia,kwa ukweli na uwazi,
Fahamu
kutufungua,maarifa waziwazi,
Bado
tunakumbukia,hayatuishi majonzi.
Kichwa
busara sawia,alikua na makuzi,
Hata
anayoongea,yamejaa uchunguzi,
Makini
anang’amua,ni kama mpelelezi,
Zile siri
azojua,ni za hatari baadhi.
Mioyo
aliinua,kwa makala changanuzi,
Tumaini
alitoa,kwa vizazi na vizazi,
Alitembea
dunia,na kutoa fafanuzi,
Wale
wanaokimbia,yanawatoka machozi.
Japo bado
apumua,alishaiacha kazi,
Anasema
inaboa,yamnyima usingizi,
Vitisho
anapokea,awekapo mambo wazi,
Kaona
kujiokoa,aache upaparazi.
Muwazi
anapokua,kuna watu awaudhi,
Wako nyuma
ya pazia,wanaleta vizuizi,
Vigogo
akiumbua,aharibu yao kazi,
Hapo kilichofatia,ni
tamati ya mtunzi.
No comments: