TUMAINI
TUMAINI
Josephat S. Hema
Hii siku
ikiisha,mimi nawe tu washindi,
Tumeyaweza
maisha,japo ni vingi vipindi,
Dhoruba
itapokwisha,tutauimba ushindi,
Tumaini
niko nawe,nawe uko na mimi.
Akufaaye
kwa dhiki,kwenye shida na raha,
Huyo ndiye
rafiki,usimwache akahaha,
Ni wewe
ninaafiki,pekeako unafaa,
Tumaini
niko nawe,nawe uko na mimi.
Zilishakuja
mvua,na jua la utosisni,
Wote
tukakimbia,ila leo naamini,
Mkono
hukuuachia,tufe wote dhorubani,
Tumaini
niko nawe,nawe uko na mimi.
Wewe
nakutegemea,nimeamua kuamini,
Chini wote
tutalia,na kicheko furahani,
Name
ninakuapia,sitakwacha asilani,
Tumaini
niko nawe,nawe uko na mimi.
No comments: