MFEREJI WA MAJI
MFEREJI WA MAJI
Josephat S. Hema
Ule mto wa
neema,katikati ya kijiji,
Wenye
wingi wa neema,daima twauhitaji,
Mto umejaa
mema,ni matamu yake maji,
Mbona sasa
unakwama,huku kwetu hauji?
Siku sasa
zayoyoma,tumepungukiwa maji,
Serikali
wanasema,tatizo ni la kijiji,
Eti miti
tunachoma,tukitafuta mtaji,
Hili
linatupa homa,bora kingine kipaji.
Ila watu
wanasema,kumezuka mfereji,
Wajanja
walishapima,katikati ya kijiji,
Hapo mali
wanachuma,kiwe chanzo cha ulaji,
Sie namba
tunasoma,wao wanajifariji.
Viongozi
wamezima,huku maji yanaisha,
Hata
tunapolalama,wanasema tunachosha,
Tumekosa
pa kusema,tumebaki sikitisha,
Hata kama
tukisema,tamaa watukatisha.
Tunataka
mtaalamu,wa kufanya utafiti,
Mfereji wa
hujumu,inapasa kudhibiti,
Hili swala
la muhimu,tukomboe wakati,
Lisije
likawa sumu,tukakosa uthabiti.
No comments: