MTEMBEZI
MTEMBEZI.
Josephat S. Hema
Mtembezi
safarini,
Bahasha
mkononi,
Kutwa
barabarani,
Ametoka
chuoni,
Mtaani
wafanya nini?
Eti msomi
wa chuo,
Mbona huna
maendeleo,
Shahada
yako sio,
Haina
maana leo,
Za
sakafuni mbio.
Ukingo
ndio kituo.
Mtembezi
mtaani,
Mara yuko
vijiweni,
Hadithi
zake makini,
Kichwa
kina madini,
Ila yuko
nyumbani.
Haimtaki
serikali,
Kwa sasa
haiajiri,
Inao watu
mahiri,
Anapaswa
kusubiri,
Hali
mekuwa shubiri.
Mtembezi
nchini,
Anaeshinda
juani,
Na ujuzi
kichwani,
Ila hakai
ofisini,
Atafanya
nini?
No comments: