TANZANIA NAKUPENDA
TANZANIA NAKUPENDA
Josephat S. Hema
Tanzania
nakupenda,moyoni umeingia,
Hata njaa
nikishinda,wapi nitakimbilia?
Uzalendo
ninalinda,hata kama ninalia,
Kuna muda
wanishinda,nami binadamu pia.
Kwanza
nilitafakari,kwa marefu na mapana,
Jinsi
ulivyo mzuri,kama kasoro hauna,
Japo nawe
una shari,ila sio nyingi sana,
Moyo
ukanishauri,nyumbani kutulizana.
Tumepewa
utulivu,wa miaka na miaka,
Hatujapewa
makovu,sisi tulisalimika,
Wala si
mengi maovu,wengi wamestaarabika,
Ila wapo
na wavivu,japo wanahesabika.
Namkumbuka
mwalimu,alivyotuunganisha,
Dini
kabila ni sumu,sisi wamoja maisha,
Kila mtu
wa muhimu,umoja kufanikisha,
Tukapata
na elimu,japo mwanzo haikutosha.
Huko nje
nikienda,Tanzania nitarudi,
Kuna
baridi huenda,muda fulani lazidi,
Ubaguzi
sitapenda,ule wa kimakusudi,
Nyumbani
wananipenda,upendo ninafaidi.
Mkacha
kwao mtumwa,alishasema mwalimu,
Hili jambo
linasemwa,tena mnalifahamu,
Ya nini
kuwa mtumwa?Nitabaki humu humu.
Hata kama
nikiumwa,unazo tiba muhimu.
Sikuachi
Tanzania,nasema hili kwa wazi,
Hili
nimeshaamua,sibadili maamuzi,
Wale
mnaokimbia,hata kwa kupiga mbizi,
Nashauri
kubakia,tuzijenge zama hizi.
No comments: