KIJIWENI
KIJIWENI
Josephat S. Hema
Ile mida
ya jioni,
Tukutane
kijiweni,
Tuongee ya
moyoni,
Jua
likishuka chini,
Tukapumzike
nyumbani.
Ni baada
ya shughuli,
Zilizotukabili,
Mchana wa
jua kali,
Tukaichosha
miili,
Hata na
zetu akili.
Tuliacha familia,
Umma
kuutumikia,
Na jamii
nzima pia,
Uzalendo
tangulia,
Kuipenda
TANZANIA.
Sasa ifike
jioni,
Pale
mgahawani,
Na kahawa
mezani,
Kilichojiri
ni nini,
Hapa kwetu
nchini.
Hii habari
ya dola,
Kupanda
kimasihara,
Ni juu
kila mara,
Ndio
chanzo cha hasara,
Na hizi
zetu hasira.
Uchumi
uliolala,
Na hizi
kodi za hila,
Tumekosa
uimara,
Sasa
twaona madhara,
Hili jambo
linakera.
Kazi tu ndio moto,
Japo
nyingi changamoto,
Na mambo
mengi ni ndoto,
Tunaishi
kwa msoto,
Sio mambo
ya kitoto.
Mpaka
tunatawanyika,
Kahawa
yamalizika,
Tena bila
muafaka,
Kesho
yatumainika,
Japo ni
ngumu kufika.
Tutakutana
na kesho,
Leo
isijekua mwisho,
Kuishi si
hitimisho,
Kesho tena
mipasho,
Kijiwe
kisiwe michosho.
Hapa ndio
kijiweni,
Kwa habari
za mjini,
Hata kote
duniani,
Na zile
mpirani,
Kesho tena karibuni.
No comments: